Saturday, February 28, 2015

SIMBA vs PRISONS, UPDATES FROM TAIFA, LEO JUMAMOSI NOV. 28 MPIRAAAA UMEKWISHAAAAAAA!

Simba inaondoka na ushindi wa mabao 5-0

KIPINDI CHA PILI, 5-0, RED CARD!!

GOOOOAAAAL 5-0
Dakika ya 81, Ramadhan 'Messi' anaifungia bao la tano Simba, shukurani kwa kazi nzuri ya Okwi aliyepiga krosi murua na kumkuta Messi katika nafasi nzuri.
OKWIII
Dk 75, Okwi anaiandikia bao la nne Simba kwa shuti nje ya box linamuacha kipa wa Prisons asijue la kufanya
Simba 4-0 Prisons
MABADILIKO
Simba wanafanya mabadiliko:
Ajibu anatoka nafasi yake inachukuliwa na Awadh Juma, Sserunkuma anatoka, yake inachukuliwa na Twaha Ibrahim  
  
PRISONS WABADILIKA
Prisons wanaonekana kubadilika kimchezo, walau sasa wanafika langoni mwa Simba, lakini hakuna la maana wamefanmya zaidi ya kuonesha ukakamavu wa kupeleka mashambulizi, lakini yote yanaishia kwa mabeki.
Ajibu wa Simba anaoneshwa kadi ya njano pamoja na beki wa Prisons, Chona. 
Chona anaonyeshwa kadi ya pili ya njano na kutolewa nje.
FOWADI YA SIMBA 
Licha ya kuongoza kwa mabao 3-0, lakini bado safu ya ushambuliaji ya Simba haina makali yoyote, Sserunkuma licha ya kuasist bao la kwanza, lakini anaonekana bado ana safari ndefu tena sana kuhimili mikikimikiki ya Kibongo.
 
 HALF TIME...SIMBA IMEISHAMLA MTU KILO TATU!!
Simba imeonekana kurudi kwenye ubora wake, baada ya kuziona nyavu za Wanajelajela wa Prisons kutoka Mbeya mara tatu mpaka sasa kipindi cha kwanza kwa mabao ya yosso hatari kwa sasa, Ibrahim Ajibu Migumba, akitumia vema kazi nzuri zilizofanywa vema na Emmanuel Okwi pamoja na Dan Sserunkuma.

Hadi dakika 45, Simba imeonekana kuutawala mchezo ambapo wapinzani wao wamefika langoni mara moja tu huku wakiwa hawajapia shuti la maana hata moja golini mwa Simba achilia mbali shuti moja lililopaa sentimita kadhaa juu.

Ajibu alianza kuzifumania nyavu mapema dakika ya 18 akimalizia vema kazi iliyofanywa na Waganda, Okwi na Sserunkuma ambapo Okwi alitoka na mpira langoni mwa Simba na kukimbia nao, kisha kumpa Sserunkuma ambaye ‘alim-setia’ Ajibu na kumchambua kipa na kuukwamisha kambani.

Ajibu alirejea tena nyavuni dakika ya 23 akimalizia mpira uliopanguliwa na kipa wa Prisons, Mohamed Yusuf aliyepangua shuti kali la Okwi, kisha Ajibu akafanya maajabu yake.

Simba walipata penalti dakika ya 41, baada ya beki wa Prisons kunawa mpira, penalti iliyopigwa kifundi na fundi Ajibu.
Hadi dakika 45, Simba 3-0 Prisons

Hali ya mashabiki

Katika kile kinachoonekana uongozi wa Simba una kazi kubwa, ni kurudisha morali ya mashabiki, kwani idadi ni ndogo sana, sana, sana ten asana kupita maelezo kwa wale wanaojua udhurio la mashabiki katika mechi za Simba.

VIKOSI

Simba: Ivo Mapunda, Ramadhan Kessy, Mohamed Hussein Tshabalala, Hasan Isihaka, Joseph Owino, Jonas Mkude, Ramadhan Singano, Said Ndemla, Dan Sserunkuma, Ibrahim Ajibu na Emmanuel Okwi.

Sub: Peter Manyika, Nassor Masoud, Issa Rashid Abdulaziz Makame, Twaha Ibrahim, Elias Maguri na Awadh Juma

Prisons: Mohamed Yussuf, Lugano Mwangama, Laurian Mpalile, James Mwasote, Nurdin Chona, Jumanne Elfadhil/ Mtei, Adam Chimbongwe, Freddy Chudu, Ibrahim Isaka, Boniface Hau na Godfrey Magetha

Sub: Enock Balagashi, John Matei, Jimmy Shoji, Julius Kwanga, Meshack Seleman, Hassan Omar na Amir Omar

No comments:

Post a Comment

POSTED TITLE

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...